YANGA YASAJILI USIKU - deepentz

Breaking News

test banner
YANGA YASAJILI USIKU

YANGA YASAJILI USIKU

Share This
Yanga imefanikiwa kupitisha jina la mshambuliaji wa zamani wa Zesco, Winston Kalengo.
Kalengo ametua Yanga baada ya jina lake kuwasilishwa katika nusu saa ya mwisho kabla ya dirisha ya usajili.
Taarifa zinaeleza, Yanga imepitisha jina hilo la Kalengo anayechukua nafasi ya Mzambia, Obey Chirwa.
Yanga imemrudisha Chirwa FC Platnums kwa mkopo, safari hii akiwa analipwa nusu mshahara na Yanga na Wazimbabwe hao watamlipa nusu mshahara.
Mjadala mkubwa kuhusiana na hilo, ndiyo ulichelewesha Yanga kuwasilisha jina hilo katika hatua za mwisho na imeelezwa Yanga wameliwasilisha katika majina ya wachezaji wao saa 5:36, ikiwa ni dakika 24 kabla ya usajili huo wa dirisha dogo kufungwa.
Pamoja na kufanya vizuri Zambia akiwa na Zesco, Kalengo aliwahi kucheza soka la kulipwa nchini Congo Brazaville na anaelezwa kuwa mkali wa kupiga mashuti, mwenye njaa ya mabao.

No comments:

Post a Comment

Featured Post

ZARI alichokifanya kwa Mtoto wa DIAMOND: kamfanyia kitendo kikubbwa.

Video hii hapa chini itakujuza zaidi kuhusiana na kisa na mkasa wa alichokiaandika zari kwa mtoto huyo hii hapa  https://youtu.be/iSLPB33Mf...

Post Bottom Ad

DEEPEN TZ

Pages